Wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo leo May 04 2016 imetangaza kuufungia wimbo wa Snura ‘chura’ kuchezwa kwenye MEDIA kuanzia leo mpaka hapo Snura atakapoifanyia marekebisho video ya wimbo huo na kutoa wimbo huo kwenye mitandao yote ya kijamii.
Sababu za kuufungia ni kinachoonekana ndani ya video ambapo pia Serikali imetangaza kusitisha maonyesho yote ya hadhara ya Snura mpaka atakapokamilisha taratibu za usajili wa kazi zake za sanaa katika baraza la sanaa la taifa BASATA.
chanzo Millardayo
0 maoni:
Post a Comment